Description
Hatua za Kiswahili Rasmi, Kitabu cha mwanafunzi ni mfululizo wa vitabu vipya vilivyoandikwa kwa ufundi kwa kufuataÂ
mtalaa mpya unaosisitiza umilisi. Vitabu hivi vitamwezesha mwanafunzi kukuza weledi wake katika stadi za kusikiliza naÂ
kuzungumza, sarufi na matumizi ya lugha, kusoma na kuandika. Vitabu hivi vina sifa zifuatazo: • Mada kuu zilizopangwa kwaÂ
kuzingatia ruwaza ya mtalaa ya Kiswahili Gredi ya 4 ili
kurahisisha utumiaji. Vipindi vilivyopangwa kushughulikia mada ndogo mbalimbali kulingana na ruwaza ya mtalaa.
Picha na michoro iliyochorwa kwa rangi za kupendeza ili kuvutia usomaji na ujifunzaji. • Maswali dodoso yanayochocheaÂ
uwezo wa mwanafunzi kufikiria na kudadisi masuala
mbalimbali. Kazi za ziada na majaribio yanayomhusisha mwanafunzi binafsi, wanafunzi wawiliwawili na wanafunzi kwenyeÂ
makundi katika shughuli ainÄ…aina. Mradi wa nyumbani unaowahusisha wazazi na walezi katika ujifunzaji wa Kiswahili na pia
kukuza uwajibikaji. · Hadithi na utajiri wa shughuli nyingine zinazokuza umilisi wa kimsingi wa lugha ya Kiswahili
na zilizooanishwa na masuala mtambuko, maadili chanya miongoni mwa masuala mengine.
Matumizi ya teknolojia kwa mfano kusikiliza sauti redioni na unasaji sauti kwa kutumia • simu na vifaa vingine vyaÂ
kiteknolojia. Mathias Momanyi ni mtafiti, mwandishi, mwalimu na mwanahabari mashuhuri. Ameandika vitabu vingi vikiwemoÂ
msururu wa Kilele cha Insha vilivyosifiwa kwa ukwasi wake wa fani na tamathali za lugha komavu. Yahya Mutuku ni mwandishiÂ
na vilevile mwalimu mwenye uzoefu na utaalamu mkubwa. Ameshiriki kikamilifu katika harakati, na mikakati ya ukuzaji waÂ
Kiswahili kupitia vipindi vya Kiswahili. Ameshirikiana na Mathias Momanyi kuandika msururu wa Kilele cha’ InshaÂ
vilivyosifiwa kwa ukwasi wake wa fani na tamathali za lugha komavu. Pia ameandika hadithi nyingi pamoja na Kamusi ya Picha.
Â
Reviews
There are no reviews yet.